Kituo cha habari cha Khaima kimeripoti kuwa mradi huo wa kujenga monoreli itakayounganisha mji wa Makka, uwanja wa Arafa na Mina imekabidhiwa kwa kampuni moja kutoka China.
Mradi huo utakaogharimu dola bilioni moja na milioni mia saba, utakamilika katika kipindi cha miaka miwili.
Kampuni hiyo pia itapewa miradi mingine ya ujenzi wa reli katika mji wa Makka ili kusahilisha harakati za mahujaji wa nyumba tukufu ya Mwenyezi Mungu. 363232