IQNA

Maombolezo ya Mtume (saw) na Imam Hassan (as) katika haram ya Imam (MA)

9:41 - February 26, 2009
Habari ID: 1748753
Maombolezo ya kifo cha Mtume Muhammad (saw) na kuuawa shahidi Imam Hassan Mujtaba (as) yamefanyika katika ziara la Imam Khomeini (MA), mwanzilishi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran mjini Tehran.
Umati mkubwa wa wananchi na wapenzi wa Watu wa Nyumba ya Mtume (saw) ulihudhuria maombolezo hayo ambayo yalifanyika siku ya Jumanne usiku.
Watu waliohudhuria maombolezo hayo hatimaye walishiriki katika swala za jamaa za Magharibi na Ishaa huku wakiwa na majonzi na huzuni kubwa.
Maombolezo kama hayo pia yamefanyika katika kaburi hilo siku ya Jumatano usiku kwa lengo la kukumbuka kuuawa shahidi Imam wa nane wa Madhehebu ya Shia, Imam Ali bin Musa ar-Ridhaa (as). 369438
captcha