Gazeti la nchi hiyo la As-Sharq limeandika kuwa wanafunzi wa kike na kiume wapatao 16,317 kutoka shule zote za serikali na zisizo za serikali watashindana katika mashindano hayo na zawadi kutolewa kwa washindi, ili kuwashajiisha wazingatie na kujifunza elimu mbalimbali za Qur'ani.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kamati inayoandaa mashindano hayo, mashandano hayo yatagawanywa katika sehemu mbili za shule bora na za binafsi na sehemu ya pili itahusiana na wanafunzi waliohifadhi juzuu saba hadi 30 za Qur'ani. 370119