Mkuu wa Kamati ya Utamaduni ya mashindano ya 14 ya Qur'ani na hadithi ya chuo cha Mustafa Ismail Piirniya amesema kuwa mashindano hayo yanajumuisha nyanja za kusoma Qur'ani, na kuhifadhi juzuu tofauti za kitabu hicho.
Ismail Piirniya amesema kuwa awamu ya mwisho ya mashindano hayo itafanyika tarehe 7, 8 na 9 za mwezi huu wa Machi yakiwashirikisha makarii kutoka nchi mbalimbali duniani ambao tayari wameanza kuwasili nchini Iran. Wasomaji Qur'ani kutoka nchi za Albania, india, Thailand, Indonesia, Nigeria, Kosovo, Tanzania, Pakistan, Uturuki, Comoro, Azerbaijan na Lebanon wamekwishawasili katika mji mtakatifu wa Qum kwa ajili ya kushiriki kwenye mashindano hayo.
Ni vyema kukumbusha hapa kuwa mashindano ya maandishi ya Qur'ani na hadithi yalianza siku tano zilizopita. 372956