IQNA

Maonyesho ya kaligrafia ya Qur'ani kufanyika Uingereza

18:25 - March 17, 2009
Habari ID: 1757150
Maonyesho ya kaligrafia ya Qur'ani Tukufu (sanaa ya kuandika vizuri aya za Qur'ani) yanatazamiwa kufanyika kesho tarehe 18 Machi katika mji wa Peterborough nchini Uingereza.
Maonyesho hayo yanasimamiwa na Kituo cha Utamaduni cha Jamhuri ya kiislamu ya Iran nchini humo.
Mabango yenye sanaa ya maandishi ya kuvutia ya Qur'ani Tukufu, Qur'ani zilizochapishwa zenye thamani kubwa, vitabu vinavyojadili maudhui ya Qur'ani na CD za Qur'ani zilizotayarishwa nchini Iran, vitaonyeshwa katika maonyesho hayo.
Mji wa Petersborough ambao una idadi kadhaa ya misiki na vituo vya Kiislamu, ni miongoni mwa miji yenye idadi kubwa ya Waislamu nchini Uingereza. 378222


captcha