IQNA

Mustafa Ismail ni nyota ya usomaji Qur'ani

14:30 - March 18, 2009
Habari ID: 1757296
Mmoja wa wahifadhi mashuhuri wa Qur'ani wa nchini Iran ameashiria kipawa kikubwa cha usomaji Qur'ani alichokuwa nacho marehemu Mustafa Ismail wa Misri na kusema kuwa alikuwa nyota ya usomaji wa kitabu hicho kitakatifu miongoni mwa wasomaji walioishi katika zama zake.
Amesema, msomaji huyo wa Misri amekuwa nyota katika fani ya usomaji Qur'ani kwa kipindi cha miaka 100 iliyopita.
Hayo yamesemwa na Sayyid Mahdi Fatimiyan, aliyehifadhi Qur'ani nzima na ambaye pia ni refa wa usomaji Qur'ani katika mazungumzo yake na shirika la IQNA. Amesema Qur'ani ni muujiza ambao una pande mbalimbali ukiwemo upande na sifa ya usomaji wake kwa sauti ya kuvutia na kwamba hadi siku ya Kiama hakuna kitabu kingine kinachoweza kushindana na kitabu hicho kitakatifu wala kudai kwamba kina uwezo wa kumuongoza mwanadamu kwa njia inayofaa. Sayyid Mahdi Fatimiyan ameendelea kusema kuwa, lahani na sauti ni moja ya sifa za kuvutia za Qur'ani na kwamba katika kipindi chote cha historia wasomaji wa kitabu hicho wameweza kuwavutia watu kimaanawi kutokana na sauti tofauti na za kuvutia za usomaji wake, jambo ambalo limewafanya wengi kusilimu. 374256
captcha