Mkutano wa kimataifa wa 'Uislamu na Juhudi za Kufungamana na Zama: Suala la Jihadi' kimepangwa kufanyika mjini Paris tarehe 10 Aprili kwa ushirikiano wa Shrika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Nchi za Kisilamu Isesco, Chuo Kikuu cha Sheria cha Paris na Shirika la Utafiti wa Jografia ya Kisasa cha mji huohuo.
Jopo la kielimu la kikao hicho ni pamoja na Abdul Aziz Othman at-Tuweijiri, Katibu Mkuu wa OIC, Jean Yves De Cara, mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Paris Charles Saint-Prot, mhadhiri wa Chuo cha Paris na mwandishi wa kitabu kiitwacho, 'Uislamu na Mustakbali wa Suna kati ya Mapinduzi na Mielekeo ya Umagharibi.'
Wataalamu wa masuala ya Kiislamu na wahadhiri kutoka katika vyuo vikuu vya nchi za Algeria, Saudi Arabia, Misri, Imarati, Ufaransa, Lebanon, Morocco na Sudan pia wamealikwa kushiriki katika kikao hicho. 382420