IQNA

Mashindano ya kila mwaka ya Qur'ani kufanyika Syria

16:27 - April 06, 2009
Habari ID: 1761156
Mashindano ya kila mwaka ya kusoma na kuhifadhi Qur'ani Tukufu yanatazamiwa kufanyika katika wiki ya mwisho ya mwezi Julai mwaka huu katika mji mkuu wa Syria, Damascus.
Washiriki katika mashindano hayo watachuana katika kuhifadhi juzuu 5, juzuu 10 na Qur'ani kamili.
Washiriki katika mashindano ya kusoma Qur'ani wanalazimika kuwa na ujuzi wa sheria za tajwidi na sauti ya kuvutia.
Mashindano hayo yanafadhiliwa na Kitengo cha Utamaduni cha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mjini Damascus. 383033
captcha