Salman al Amri ambaye ni miongoni mwa wasimamizi wa mashindano hayo amesema kuwa awamu ya kwanza ya mashindano ya Amir Sulaiman itafanyika katika maeneo mbalimbali ya Saudi Arabia na washindi watano wa kwanza watafaulu kuingia fainali.
Mashindano hayo ya kuhifadhi Qur'ani yanasimamiwa na Idara ya masuala ya Kiislamu ya Saudia.
Watayarishaji wa mashindano hayo wamewahidi kutoa zawadi nono kwa washindi wa mashindano hayo.
Watu wote wanaotaka kushiriki kwenye mashindano hayo wanalazimika kuwa wamejiandikisha kufikia tarehe 18 Aprili. 386015