Hayo yamesemwa na mtengeneza filamu maarufu wa Iran Majid Majidi ambaye ameongeza kuwa Wamagharibi wanapaswa kuonyeshwa picha tofauti na ile inayoonyeshwa kwenye vyombo vya habari vya nchi zao kuhusu Iran. Amesisitiza kuwa vyombo hivyo vya habari vinapuuza historia na utamaduni tajiri wa Iran wakati vinapozungumzia nchi hiyo.
Majid Majidi amesema kuwa si kazi sahihi kutazama kila kitu kwa kutumia jicho la masuala ya kisiasa na kwamba mwenendo huo ndio sababu ya kuonyeshwa picha isiyokuwa sahihi kuhusiana na Iran na watu wake katika vyombo vya habari. 386215