IQNA

Mkutano wa kimataifa wa Swala na Qur'ani kufanyika Tehran

15:02 - April 13, 2009
Habari ID: 1764344
Mkutano wa kwanza wa kimataifa wa Swala na Qur'ani unatazamiwa kufanyika msimu wa mapukutiko wa mwaka huu katika Chuo Kikuu Huria cha Kiislamu cha Azadi mjini Tehran.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kusimamisha Swala ya Chuo Kikuu Huria cha Kiislamu cha Azadi Aliridha Salihi amesema kuwa mkutano huo utafanyika kwa lengo la kujadili na kubadilisha tajiriba kati ya wanachuo wa Kiislamu katika medani ya Qur'ani na swala. Ameongeza kuwa kwa sababu hiyo Chuo Kikuu Huria cha Kiislamu cha Azadi ambacho ni Mwenyekiti wa Baraza la Utendaji la vyuo vikuu vya ulimwengu wa Kiislamu, kimeazimia kuitisha mkutano huo wa kimataifa wa Swala na Qur'ani kama hatua yenye taathira kubwa katika uwanja huo.
Amesema maandalizi ya mkutano huo yamekwishaanza.
Salihi amesema kuwa mkutano huo utajadili maudhui za Qur'ani, swala na Ahlubaiti wa Mtume Muhammad (saw). 386767

captcha