IQNA

Chuo Kikuu cha Indiana, mwenyeji wa vitabu vya dhahabu vya Kiislamu

13:05 - April 14, 2009
Habari ID: 1764724
Maonyesho ya vitabu vya Kiislamu vilivyonakshiwa kwa dhahabu yamekuwa yakiendelea katika Chuo Kikuu cha Indiana nchini Marekani tokea tarehe 6 Machi.
Kwa mujibu wa tovuti ya IUPress, jumba la maonyesho ya kale la chuo hicho limeandaa maonyesho maalumu ya sanaa ya nakshi ya dhahabu ambapo vitabu vipatavyo 50 vilivyonakshiwa na kupakwa rangi ya dhahabu vinaonyeshwa.
Vyombo na zana zinazotumika katika sanaa hiyo tokea karne ya tisa hadi leo vinaonyeshwa katika maonyesho hayo yanayoendelea hadi tarehe 10 Mei. 387018
captcha