IQNA

Maonyesho ya irfan ya Kiislamu mjini New York

12:50 - April 14, 2009
Habari ID: 1764728
Kazi za sanaa inayohusiana na irfan ya Kiislamu zitaonyeshwa katika jumba la maonyesho ya mambo ya kale la Brookline la mjini New York Marekani tokea tarehe 5 Juni hadi 6 Septemba mwaka huu.
Kwa mujibu wa tovuti ya Artdaily athari au kazi zitakazowasilishwa katika maonyesho hayo zitasisitiza juu ya irfani ya Kiislamu kwa kujadili masuala kama vile nuru katika irfani ya Kiislamu, sifa za usufi, mashairi ya kiirfani na athari za irfani ya zamani na ya zama hizi. Mashairi ya Maulana yaliyotarjumiwa kwa lugha ya Kiingereza ni miongoni mwa mambo yatakayoonyeshwa katika maonyesho hayo. 387495
captcha