IQNA

Mkutano wa Waislamu wa Limousin

9:16 - April 15, 2009
Habari ID: 1765117
Kikao cha kwanza cha kila mwaka cha Waislamu wa jimbo la Lomousin nchini Ufaransa ambacho kimeandaliwa na Jumuiya ya Udugu ya Limoges kitafanyika katika mji huo tarehe 9 Mei.
Kwa mujibu wa Saphirnews, kikao hicho kitafanyika kwa ushirikiano wa jumuiya za Kiislamu za miji ya Brive-la-Gaillarde na Guéret.
Maonyesho mbalimbali yanayohusiana na ulimwengu wa Kiislamu yataandaliwa, na makundi ya kiutamaduni na sanaa kutekeleza ratiba mbalimbali za burudani. 388126
captcha