IQNA

Maonyesho ya vitabu vya Kiislamu na Kiarabu nchini Senegal

9:39 - April 18, 2009
Habari ID: 1765981
Duru ya pili ya maonyesho ya vitabu vya Kiarabu na Kiislamu itafanyika tarehe 23 hadi 26 za mwezi huu wa Aprili katika mji wa Lugha nchini Senegal. Vikao mbalimbali vya mijadala vinavyohusiana na maonyesho hayo vitafanyika pembeni ya maonyesho hayo.
Oustaz Cheikh Seck, Imam wa Swala ya Ijumaa ya mji huo na ambaye pia ni miongoni mwa watayarishaji wa maonyesho hayo ameashiria umuhimu wa maonyesho hayo na kusisitiza kwamba yametayarishwa ili kuarifisha masuala ya kielimu na kidini ya waandishi wa Kiarabu na Kiislamu na hasa wa Senegal kwa wanafunzi na watafiti wa masuala ya kielimu ili waweze kufikia kirahisi marejeo ya kuwawezesha kunyanyau viwango vyao vya maarifa na elimu. Amesema pia vitabu vilivyoandikwa kwa lugha ya Kisenegali na ambavyo vimetarjumiwa kwa lugha za Kiarabu na Kifaransa pia vitaonyeshwa katika maonyesho hayo. 389538
captcha