IQNA

Sherehe za kuwatuza mabinti waliohifadhi Qura'ni nchini Saudi Arabia

13:58 - April 23, 2009
Habari ID: 1768742
Sherehe za kushukuru na kuwatuza mabinti wa Kiislamu waliohifadhi Qur'ani tukufu zilianza siku ya Jumatano katika ukumbi wa Farhati huko katika mji mtakatifu wa Makka ambapo zimehudhuriwa na mwanamfalme Swita bint Abdallah bin Abdul Aziz.
Kwa mujibu wa gazeti la al-Madina linalochapishwa nchini Saudi Arabia, sherehe hizo zimeandaliwa na Jumuiya ya Masuala ya Kheri ya Kuhifadhi Qur'ani Tukufu ya Saudi Arabia kwa lengo la kuwashajiisha wasichana wajishughulishe na masuala ya Qur'ani. As-Sheikh Hamud bin Atiq al-Maabadi, mmoja wa wakuu walioandaa sherehe hizo amesema kuhusiana na suala hilo kwamba, sherehe hizo zitajumuisha visomo vya watu waliohifadhi Qur'ani, hotuba za watu waliohitimu masomo yao katika jumuiya hiyo, kuwasilishwa rekodi ya shughuli zilizotekelezwa na jumuiya hiyo pamoja na kutolewa zawadi kwa watu waliofanya vyema katika uhifadhi wa Qur'ani Tukufu. 392883
captcha