IQNA

Waliofikia hatua ya mwisho ya mashindano ya Qur'ani ya Amir Salman wajulikana

8:06 - April 25, 2009
Habari ID: 1769091
Wavulana na wasichana 91 wamefanikiwa kufikia hatua ya mwisho ya duru ya 11 ya mshindano ya kitaifa ya kuhifadhi Qur'ani Tukufu ya Zawadi ya Amir Salman bin Abdul Aziz ambayo itafanyika tarehe Nne Mei mjini Riyadh nchini Saudi Arabia.
Kwa mujibu wa gazeti la al-Jazeera linalochapishwa mjini Riyadh, mashindano hayo yataendelea kwa muda wa siku kumi katika hoteli ya al-Izdihar Huleidi katika mji huo.
Abdul Aziz bin Adbul Rahman, Katibu wa Mashindano ya Qur'ani katika Wizara ya Wakfu na Masuala ya Kiislamu ya Saudi Arabia amesema kuhusiana na suala hilo kwamba, baada ya kupita miaka 11 tokea kufanyike duru ya kwanza ya mashindano hayo, mashindano ya hivi sasa yameshuhudia mapokezi makubwa zaidi ya washiriki. Amesema kuwa mashindano hayo yatafanyika katika hatua tatu tofauti za kieneo, kimkoa na kitaifa.393668
captcha