Kundi moja la walemavu wa Ulaya wataelekea katika mji wa Gaza mapema mwezi ujao wa Mei kwa lengo la kuonyesha mfungamano wao na wakazi wa mji huo na hasa walemavu na majeruhi, wahanga wa mashambulio ya mauji ya umati yaliyotekelezwa hivi karibuni na utawala haramu wa Israel dhidi ya wakazi wasio na hatia wa Ukanda wa Gaza.
Kwa mujibu wa tovuti ya Palestine-info, Rami Abdou anayesimamia misafara ya walemavu wa Ulaya amesema kuhusiana na suala hilo kwamba, walemavu hao wa ulaya watafanya safari mjini Gaza ili kutangaza mfungamano wao na wahanga wa mashambulio hayo na pia kuchunguza njia za kuwafikishia misaada ya kibinadamu.
Ameongeza kuwa madaktari wengi wataalamu wanaandamana na walemavu hao katika msafara mkubwa wa malori yaliyobeba misaada ya chakula na madawa na kwamba hivi karibuni watavuka mji wa Alexandria nchini Misri wakielekea katika Ukanda wa Gaza. 395513