Gazeti la al Khalij limeandika kuwa Mkuu wa kamati hiyo Ibrahim Bumalha amesema kuwa mashindano ya sauti nzuri zaidi ya kusoma Qur'ani yanaanza leo katika ukumbi wa Islah.
Ameongeza kuwa mashindano hayo yatakayoendelea kwa kipindi cha siku tano yatahudhuriwa na wajumbe wote wa kamati inayosimamia mashindano ya kimataifa ya Qur'ani ya Zawadi ya Dubai. Amesema kuwa mashindano ya sauti nzuri ya kusoma Qur'ani ni moja ya sehemu mpya za mashindano ya kimataifa ya Qur'ani Zawadi ya Dubai. 397902