Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA katika eneo la Kusini Mashariki mwa Asia,mbali na Jumuiya ya Maqari wa Thailand, mashindano hayo pia yamedhaminiwa na Jumuiya ya Maqari Wanaowaunga Mkono Watoto Mayatima, Chuo cha Kiislamu cha Bangkok na Benki ya Kiislamu ya Thailand.
Mashindano hayo ya siku mbili yatakayowajumuisha waliohifadhi Qur'ani katika viwango vyote yatafanyika katika ukumbi wa Chuo cha Kiislamu cha Bangkok.
Imearifiwa kuwa, washindi katika mashindano hayo watashiriki katika Mashindano ya Kimataifa ya Kuhifadhi Qur'ani ya Saudi Arabia yatakayofanyika katika mji mtakatifu wa Makka. 396870