IQNA

Maqari wa Kimataifa wasoma Qur'ani katika maonyesho ya vitabu Tehran

11:50 - May 07, 2009
Habari ID: 1775098
Maqari maarufu wa Iran watashiriki katika vikao vya kusoma Qur'ani Tukufu katika maonyesho ya kimataifa ya vitabu ya Tehran.
Muhammad Taqi Mirzajani, afisa wa mawasiliano katika Baraza Kuu la Qur'ani amemwambia mwandishi wa IQNA kuwa: ‘Kwa ushirikiano wa waandalizi wa maonyesho na Baraza Kuu la Qur'ani, maqari wa kimataifa watasoma Quran katika eneo la maonyesho, Ukumbi Mkubwa wa Swala wa Imam Khomeini (SA), kwa siku kumi za maonyesho kuanzia tarehe 6 Mei’.
Ameongeza kuwa, tilawa ya Qur'ani Tukufu, adhana, na usomaji dua wakati wa adhuhuri na magharibi pamoja na kuongoza sala za Jamaa ni kati ya ratiba zilizoandaliwa na Baraza Kuu la Qur'ani katika maonyesho ya vitabu mwaka huu mjini Tehran. 400745
captcha