IQNA

Waliofuzu katika mashindano ya kuhifadhi Quran Kuwait wazawadiwa

11:10 - May 09, 2009
Habari ID: 1775710
Waliofuzu katika mashindano ya kumi na mbili ya Quran Tukufu ya ‘Hayati Mohammad Abdulmohsen al Kharafi’ wamezawadiwa katika sherehe zilizohudhuriwa na Jasim Al Kharafi, mbunge wa zamani wa Kuwait.
Kwa mujibu wa gazeti la Al Watan, hafla hiyo imehudhuriiwa na Maqari na Mahafidh elfu tano kutoka mataifa mbali mbali ambao ni vijana wakiwemo mabanati na wavulana.
Jasim al Kharafi amesema mashindano hayo yanafanyika kwa lengo la kuwahimiza vijana na mabarobaro kuhifadhi Kitabu Kitakatifu cha Mwenyezi Mungu. Amesema mojawapo ya njia pekee ambazo vijana wanaweza kunusurika kutokana na maovu yanayoandamana na utandawazi ni kufanyika mashidano kama hayo ya Quran. Amemuomba Mwenyezi Mungu ampe taufiki ili mashindano hayo yaendelee. 401252

captcha