IQNA

Kukamilika mashindano ya kimataifa ya Qur'ani nchini Bahrain

12:26 - May 09, 2009
Habari ID: 1775777
Sherehe za kushukuriwa na kutunukiwa zawadi washindi wa kusoma na kuhifadhi Qur'ani katika duru ya kumi ya mashindano hayo ya kimataifa yaliyomalizika hivi karibuni nchini Bahrain chini ya anwani Dhikrul Hakim zilifanyika siku ya Alkhamisi katika mji mkuu wa nchi hiyo Manama.
Kwa mujibu wa gazeti la nchi hiyo la al-Wasat wasomi mashuhuri wa Qur'ani kutoka nchi za Saudi Arabia, Kuwait, Bahrain, Qatar na Pakistan walishiriki katika mashindano hayo wakiwa katika makundi mawili ya watoto na watu wazima ambao wote walikuwa ni wanaume. Mashindano hayo yaliyoanza tarehe Pili Mei yameandaliwa na jumuiya ya Qur'ani ya Dhikrul Hakim. Ayatullah Sayyid Abdallah al-Ghureifi, mwanazuoni mashuhuri wa Kishia wa Bahrain alishiriki katika sherehe hizo. Mashindano ya uandishi wa mkono wa lugha ya Qur'ani pia yaliandaliwa pambizoni mwa mashindano hayo ambapo Ali Abdul Wahid As-Shahabi ndiye aliyeibuka msindi wa mashindano hayo. 401604
captcha