Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA nchini Syria, kongamano hilo litaendelea kwa siku tatu na litajumuisha washiriki kutoka nchi kama vile Malaysia, Misri, Saudi Arabia, Libya, Uturuki, Sudan, Jordan, Palestina, Uzbekistan na Pakistan.
Kongamano hilo limedhaminiwa na Jumuiya ya Wahandisi wa Syria.
Washiriki wa mkutano huo wa kitaalamu watajadili masuala kuhusu ulindaji mazingira na uhusiano wa suala hilo na teknolojia chini ya anuani ya: 'Kulinda Mazingira na Teknolojia'. 401693