Kwa mujibu wa gazeti la Khaleej Times, kwa mara nyingine tena kamati hiyo ya Umoja wa Mataifa imeutaka utawala wa Israel kushirikiana nayo kuhusiana na suala hilo. Mwezi uliopita utawala wa Tel Aviv ulitangaza kwamba hautashirikiana kwa nia yoyote ile na kamati hiyo. Richard Goldstone, Mwendesha Mashtaka wa zamani wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai na ambaye ndiye mkuu wa hivi sasa wa kamati hiyo ya wataalamu wanne, ambayo ilibuniwa mwezi uliopita kwa ajili ya kufuatilia jinai za utawala wa Israel katika Ukanda wa Gaza, amesema kuwa uchunguzi wa kisheria na usiopendelea upande wowote ule kuhusiana na suala hilo utakuwa ni kwa mslahi ya wote, na pia kwa faida ya kuimarishwa amani na usalama katika Mashariki ya Kati. Katika upande wa pili, shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limetangaza kwamba utawala wa Israel ulitekeleza jinai za kivita dhidi ya Wapalestina kwa kutumia silaha zilizopigwa marufuku kimataifa za fosforasi nyeupe dhidi yao. 402032