IQNA

Mazoezi yanamwezesha msomaji kudhibiti kisomo chake

9:39 - May 10, 2009
Habari ID: 1776062
Msomaji mmoja mashuhuri wa Qur'ani nchini Iran anaamini kwamba mazoezi ya kudumu ya usomaji wa kitabu hicho humfanya msomaji kuwa na kipawa cha na uwezo wa kudhibiti usomaji wa kitabu hicho kitakatifu.
Hayo yamesemwa na Amin Puya ambaye ameongeza kuwa tunapasa kujifunza usomaji sahihi wa Qur'ani kwa kusoma misingi na kanuni sahihi za usomaji kitabu hicho. Akizungumza hivi karibuni mbele ya wapenzi wa Qur'ani mjini Tehran, Puya amesema kuwa usikilizaji wa visomo vya Qur'ani vya wasomaji mashuhuri wa kitabu hicho cha wahyi, na hasa cha Mahmoud Khalil al-Huswari, humsaidia sana msomaji kusoma kwa njia sahihi kitabu hicho. Amesema, kisimo cha tartil na tajweed cha msomaji huyo husaidia sana katika kumwezesha msomaji kusoma vyema aya za Qur'ani Tukufu. 402103
captcha