IQNA

Warsha ya teknolojia ya mawasiliano katika uchumi wa Kiislamu

12:32 - May 12, 2009
Habari ID: 1777357
Warsha wa mafunzo kuhusu 'Nafasi ya Teknolojia ya Mawasiliano Katika Uchumi wa Kiislamu' itafanyika mwezi ujao mjini Karachi Pakistan.
Kwa mujibu wa mtandao wa intaneti wa Alhudacibe, lengo la warsha hiyo ya mafunzo ni kuchunguza njia za kutumia teknolojia ya mawasiliano kwa mujibu wa sheria za Kiislamu pamoja na kuboresha utendaji kazi wa kiteknolojia wa benki na taasisi za kifedha za Kiislamu.
Warsha hiyo inafanyika kwa udhamini wa Kituo cha Uchumi na Benki za Kiislamu cha Pakistan. Wahadhiri katika warsha hiyo ni wataalamu wa kompyuta na teknolojia ya mawasiliano. 403597
captcha