IQNA

Wanachuo wafuzu katika chuo cha kuhifadhi Quran Uturuki

12:31 - May 12, 2009
Habari ID: 1777359
Kundi la kwanza la Mahafidh wa Qur'an Tukufu limekamilisha masomo na kufuzu katika Msikiti wa Hafidh Ali huko Istanbul Uturuki.
Kwa mujibu wa ukurasa wa mtandao wa habari wa Zaman, wanachuo saba katika vikao hivyo vya kuhifadhi Quran Tukufu walitunukiwa vyeti katika hafla iliyohudhuriwa na maafisa wa serikali ya Uturuki pamoja na wageni kutoka nchi za Kenya, Ethiopia, Tanzania na Congo.

Ustadh Jamil Toker aliyeendesha darasa hizo anasema: 'Mafunzo haya ya kuhifadhi Quran Tukufu yamechukua kipindi cha mwaka moja na walio shiriki walikuwa na umari wa miaka 15-20. Wamefanikiwa katika mtihani wa kuhitimisha muhula wote wa masomo na hivyo kupokea cheti cha kuhifadhi Quran kikamilifu'.
Ameongeza kuwa, hivi sasa kuna wanachuo 33 katika chuo hicho ambao wanatazamiwa kuhitimu mwaka ujao. Ustadh Jami Toker amesema kuwa pembeni mwa mafunzo ya Quran kuna masomo mengine ya masuala ya akhlaqi. 403514

captcha