Vituo viwili vipya vya mafunzo ya Quran Tukufu vijulikanavyo kama 'Sayyeda Ruqaiya (SA) ' na 'Abdulla bin al Hussein (AS) vimefunguliwa na Taasisi ya Misaada ya Imam Ali (AS) chini ya usimamizi wa Ayatollah Mohammad Taqi Modarresi, mwanazuoni wa ngazi za juu wa Kishia katika mji mtakatifu wa Karbala nchini Iraq.
Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, taasisi hizo mbili ziko katika maeneo ya al Nasir, na al Amal mjini Karbala na zinajishughulisha na mafunzo ya kusoma na tafsiri ya Qur'an Tukufu kwa watoto na vijana. Taasisi hizo pia zinatoa mafunzo ya lugha za Kiarabu na Kiingereza pamoja na hesabu.
Mwanachama wa Taasisi ya Misaada ya Imam Ali (AS), Abdulgani Karbalai amesema vituo hivyo viwili vitakuwa na wanafunzi takribani 55. Ameongeza kuwa masomo yote yanatolewa bila malipo.
405386