IQNA

Kambi ya Quran kwa wanafunzi 2000 mjini Tehran

14:08 - May 18, 2009
Habari ID: 1779619
Kambi ya wanafunzi 2000 waliotia fora katika mashindano ya Quran na Sala mwaka huu watashiriki katika kambi maalumu masomo ya Quran katika mji mkuu wa Iran, Tehran mwezi Julai.
Huriya Aqbani afisa anayeshusika na masuala ya Quran na Uislamu katika idara ya elimu mkoani Tehran amemuambia mwandishi wa IQNA kuwa kambi hiyo ya Qurani itajumuisha pia masuala mbali mbali ya kielimu na kiutamaduni.
Amesema katika kambi hiyo kutakuwa na vikao maalumu ya kujikurubisha zaidi na Quran Tukufu. Mbali na darasa maalumu za Quran kutakuwa pia na mafunzo kuhusu Imam Mahdi, sheria za kidini, utumizi wa kompyuta,uandishi habari n.k. 406255
captcha