Waandaaji wa maadhimisho hayo wanasema kuwa yana umuhimu mkubwa kwa kutilia maanani kwamba mafundisho yenye thamani kubwa ya kitabu hicho kitakatifu humletea mwanadamu saada ya humu duniani na huko Akhera pamoja na kumkinga na machafu na vilevile maovu ya kimaadili humu duniani. Akizungumzia maadhimisho hayo, Hamid Abud Abbas, Mkuu wa Chama cha Kiislamu katika eneo la an-Naqab amesema kuwa lengo la kufanyika maadhimisho hayo ni kuwashajiisha wananchi wa Palestina na hasa tabaka la vijana kuhifadhi kitabu hicho kitakatifu na kudiriki maana ya mafundisho yake yenye thamani kubwa kwa mwanadamu. 406893