Kikao cha nane cha kimataifa cha jumuiya za kidini zinazosimamia Mashirika ya kifedha ya Kiislamu kilianza siku ya Jumanne katika mji wa Manama, Bahrain. Kwa mujibu wa shirika rasmi la habari la nchi hiyo GNA, wawakilishi wa jumuiya za kidini zinazosimamia shughuli za kiuchumi na miamala ya kibiashara ya mashirika ya kifedha na benki za Kiislamu wanashiriki katika kikao hicho.
Kikio hicho cha siku mbili, kitajadili changamoto zinazoyakabili mashiriki ya kifedha ya Kiislamu, ustawi wa sekta ya benki za Kiislamu duniani na kuimarisha usimamizi wa sheria za Kiislamu juu ya mashirika na benki za Kiislamu. Uchunguzi wa namna ya kuimarisha usimamizi wa benki kuu za nchi za Kiislamu kwa benki na mashirika ya kifedha ya Kiislamu, ni jambo jingine litakalojadiliwa na kuchunguzwa kwa kina na kikao hicho. Kikao hicho kimeandaliwa na Benki Kuu ya Bahrain kwa ushirikiano wa Benki ya Ustawi ya Kiislamu. Kikao hicho kilimalizika jana Alkhamisi kwa kutolewa taarifa ya kufuatilia masuala yaliyoafikiwa. 408278