Mkutano huo utakaoendelea kwa siku tatu unahudhuriwa na zaidi ya viongozi na Waislamu 500 kutoka maeneo yote ya Marekani.
Mkutano huo unajadili masuala mbalimbali ya Waislamu wa Marekani.
Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Uhusiano wa Uislamu na Marekani CAIR Nihad Awadh amehutubia kikao cha ufunguzi wa mkutano huo akiashiria ongezeko la wimbi la chuki na uhasama dhidi ya Uislamu na akasema, njia pekee ya kukabiliana na hujuma hiyo ni kueneza maarifa na elimu kati ya wafuasi wa dini mbalimbali. Amesema kuwa kuna udharura wa kuwaelimisha watu kuhusu Uislamu na kuwafahamisha kwamba ni dini ya amani, uadilifu na upendo.
Mkutano huo utakalimisha shughuli zake kesho Jumapili. 431688