IQNA

Kongamano la Kimataifa la Qur'ani Tukufu kufanyika India

16:27 - March 27, 2010
Habari ID: 1900087
Kongamano la Kimataifa la Qur'ani Tukufu litazamiwa kufanyika tarehe 29 mwezi Aprili mwaka huu katika mji wa Trivandrum makao makuu ya jimbo la Kerala nchini India.
Kongamano hilo litahudhuriwa na wasomi, wanazuoni na wanafikra wa Kiislamu kutoka nchi mbalimbali duniani katika Chuo Kikuu cha Kerala. Mkuu wa Kitengo cha Lugha ya Kiarabu cha Chuo Kikuu cha Kerala A. Nizarudeen amesema mada kuu ya kongamano hilo ni nafasi ya lugha ya Qur'ani Tukufu katika elimu na sayansi.
Masuala mengine yatakayochunguzwa katika kongamano hilo la kimataifa ni muundo wa Qur'ani Tukufu, tafsiri za Qur'ani katika vipindi mbalimbali, njama za kupotosha maandiko ya Qur'ani, kaligrafia ya Qur'ani, Qur'ani za digitali na kadhalika.
Kongamano hilo pia litafanyika sambamba na vikao vya kiraa ya Qur'ani, mashindano na maonyesho ya kitabu hicho kitukufu cha Mwenyezi Mungu. 555063



captcha