IQNA

Mashindano ya kila mwaka ya Qur'ani yaanza Libya

13:58 - April 12, 2010
Habari ID: 1906016
Mashindano ya 21 ya Qur'ani Tukufu yameanza leo katika mji wa Tripoli nchini Libya. Mashindano hayo ambayo hufanyika kila mwaka yataendelea kwa kipindi cha siku tatu.
Gazeti la al Fajr el Jaded limeandika kuwa mashindano hayo yanasimamiwa na Idara ya Waqfu ya jiji la Tripoli ikishirikiana na vituo 50 vya mafunzo ya Qur'ani.
Mashindano hayo yanajumuisha sekta za kuhifadhi Qur'ani nzima, juzuu 15 na juzuu saba za mwisho za kitabu hicho.
Mkuu wa Idara ya Waqfu ya Tripoli amesema kuwa lengo la mashindano hayo ya Qur'ani ni kuhamasisha vijana kuhifadhi Qur'ani na kuwatayarisha kwa ajili ya mashidano ya kimataifa ya kitabu hicho kitakatifu. 560475
captcha