IQNA

Mwanamke mwenye umri wa miaka 100 ashinda mashindano ya Quran Saudi Arabia

22:55 - July 28, 2010
Habari ID: 1963571
Ajuza mwenye umri wa miaka 100 nchini Saudi Arabia katika eneo wa Al Bashair amefanikiwa kupata nafasi ya kwanza katika mashindano ya kuihifadhi Quran Tukufu maalumu kwa wanawake.
Kwa mujibu wa duru za habari nchini Saudia, mashindano yamefanika kwa himaya ya Jumuiya ya Kuhifadhi Quran ya eneo la Al Bashair na yalikuwa katika kiwango cha kuhifadhi Juzuu 10 za Quran Tukufu kwa kuzingatia kanuni za Tajweed. Ajuza huyo mwenye umri wa miaka 100 ameweza kujibu maswali yote bila kufanya kosa lolote katika mashindano hayo.
622530
captcha