IQNA

Iran kuandaa hafla 30 za Wiki ya Quran katika nchi kadhaa duniani

17:44 - August 09, 2010
Habari ID: 1970081
Shirika la Iran la Utamaduni na Mahusiano ya Kiislamu ICRO limetangaza kuwa litaandaa hafla 30 za Wiki za Quran katika nchi mbali mbali duniani katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Mkuu wa Masuala ya Utamaduni katika ICRO Mohsen Pakayeen amesema maqari 50 wa kimataifa pamoja na makundi 20 ya Qaswida yatatumwa katika nchi mbali mbali katika Mwezi wa Ramadhani. Ameongeza kuwa ICRO inasimamia kitengo cha wachapishaji wa kimataifa katika Maonyesho ya 18 ya Kimataifa ya Quran Tukufu yaliyoanza Jumamosi usiku mjini Tehran. Maonyesho hayo ambayo yana washiriki kutoka nchi 25 duniani yatamalizika tarehe 23 ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
628083
captcha