IQNA

Algeria yaandaa mashindano ya kimataifa ya Qurani

16:01 - August 18, 2010
Habari ID: 1976514
Mashindano ya saba ya “Zawadi ya Kimataifa ya Qiraa, Tartil na Tafsiri ya Qurani Tukufu” yatafanyika kuanzia tarehe 20 hadi 26 ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani nchini Algeria.
Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, Idara ya Miongozo ya Kidini na Mafundisho ya Qurani katika Wizara ya Waqfu na Masuala ya Kiislamu ya Algeria imetoa taarifa na kusema: “Mashindano haya yatafanyika chini ya usimamizi wa Rais wa Algeria Abdulaziz Bouteflika na yatashirikisha nchi 41 wanachama wa Jumuiya ya Nchi za Kiislamu . Washiriki watakuwa chini ya umri wa miaka 25”.
Taarifa hiyo imeongeza kuwa : “Jopo la majaji litajumuisha Maustadhi watatu kutoka Algeria, Libya na Iran”.
Zawadi za mashindano hayo ya kimataifa ya Quran nchini Algeria yatakuwa kama ifuatavyo: Nafasi ya kwanza Milioni Dinari milioni moja, nafasi ya pili Dinari laki nane na nafasi ya tatu dinari laki sita.
636244
captcha