IQNA

Kumalizika duru ya 15 ya mashindano ya Qur'ani nchini Bahrain

11:33 - August 22, 2010
Habari ID: 1978390
Duru ya 15 ya mashindano ya kusoma na kufasiri Qur'ani Tukufu ambayo yamekuwa yakiendelea huko Manama mji mkuu wa Bahrain yamepangwa kumalizika tarehe 27 ya mwezi huu wa Agosti.
Kwa mujibu wa shirika rasmi la habari la nchi hiyo BNA, Bwana Farid al-Fatih, Naibu Waziri wa Sheria na Masuala ya Kiislamu wa Bahrain amesema kuhusiana na suala hilo kuwa sherehe za kufunga mashindano hayo zitafanyika katika msikiti wa Ahmad al-Fatih. Ameongeza kuwa Khalid bin Ali al-Khalifa, Waziri wa Sheria na Masuala ya Kiislamu wa Bahrain atahudhuria sherehe hizo.
Mashindano hayo yamewashirikisha vijana 104 wa kike na kiume. Washindi wa watapewa zawadi nono katika sherehe hizo. 638245
captcha