Mashindano hayo yameandaliwa na Kituo cha Shia Ithna-Asheri kilichoko katika mji huo. Kwa mujibu wa tovuti ya kituo hicho 'Sijny' mashindano hayo yameandaliwa kwa madhumuni ya kunyanyua kiwango cha maarifa ya Qur'ani katika familia za Waislamu na kuwashajiisha wawe na hamu ya kusoma na kuzingatia kitabu hicho kitakatifu.
Kituo kilichotajwa cha Kiislamu kimekuwa kikiweka maswali ya Qur'ani katika kurasa za tovuti yake na kuwataka walio na hamu ya kuyajibu, wayajibu na kisha kuchunguzwa na wasimamizi husika wa kituo hicho. Washindi wamepangiwa kutunukiwa zaidi katika siku ya Idulfitr. 638283