IQNA

Kulaaniwa kuchomwa moto Qur'ani nchini Marekani

11:12 - August 25, 2010
Habari ID: 1980902
Jumuiya ya Kimataifa ya Dini kwa ajili ya Amani, ambayo ni taasisi kubwa zaidi ya mjumuiko wa dini tofauti duniani imelaani vikali hatua ya kasisi mmoja wa jimbo la Florida la nchini Marekani ya kuainisha tarehe 11 Septemba kuwa ni siku ya kuchoma moto kitabu kitakatifu cha Waislamu Qur'ani.
Kwa mujibu wa gazeti la as-Sharqul Ausat, taasisi hiyo ya kimataifa iliyo na makao makuu yake mjini New York Marekani, imetoa taarifa ikisema kuwa hatua ya kasisi huyo ya kutaka kuchoma moto hadharani Qur'ani Tukufu ni kitendo hatari, kosa kubwa na dharau ya wazi kwa matukufu ya kidini.
Taarifa hiyo imesisitiza kwamba viongozi wa madhehebu zote za Kikristo pamoja na wafuasi wa dini hiyo kote ulimwenguni wanapinga na kulaani vikali kitendo hicho cha dharau. Tunakumbusha hapa kuwa hatua ya kasisi huyo imeamsha hasira kubwa ya Waislamu, taasisi za Kiislamu pamoja na wafuasi wa dini mbalimbali duniani. 641195
captcha