IQNA

Tamasha la kuwaenzi Mahafidhi wa Qur'ani Misri

11:33 - September 07, 2010
Habari ID: 1989143
Tamasha la kila mwaka la kuwaenzi Mahafidhi wa Qur'ani Tukufu limefanyika nchini Misri na kuhudhuriwa na Mahafidhi 400 wa Qur'ani Tukufu.
Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, tamasha hilo limefanyika katika mji wa Al Saf kwa himaya ya jumuiya ya Qur'ani ya mji huo. Tamasha hilo la Jumapili lilihudhuriwa na wanazuoni wa Chuo Kikuu cha al Azhar na wawakilishi wa Wizara ya Wakfu na Masuala ya Kiislamu ya Misri na vilevile maulama wa Qur'ani wa Misri.
Mkuu wa Jumuiya ya Qur'ani ya mji wa Al Sad Sami Ismail Elam amesema: "Mahafidhi wa Qur'ani wametunukiwa nishani na zawadi za kifedha na 100 kati yao wametunukiwa zawadi maalumu".
649815

captcha