Kwa mujibu wa shirika la Dunyabulteni kongamano hilo la siku tatu litafunguliwa kwa hotuba ya Ekmeleddin Ihsanoglu, Katibu Mkuu wa OIC na litachunguza masuala mbalimbali yanayohusiana na maisha ya Waislamu nchini Marekani.
Masuala mengine yatakayojadiliwa ni pamoja na nafasi ya OIC ulimwenguni na athari zake kwa Waislamu wa Marekani, siasa za nje za Marekani na ulimwengu wa Kiislamu, taathira ya Uislamu kwa muundo wa kijamii wa Waislamu wa Marekani na taswira kuhusu mustakbali wa masomo, utamaduni na siasa za Waislamu wa nchi hiyo.
Wawakilishi wa jumuiya mbalimbali za Kiislamu za Marekani zikiwemo za Baraza la Uhusiano wa Uislamu na Marekani CAIR, Muungano wa Waislamu wa Marekani Kaskazini MANA, wanafikra na wanazuoni wa Kiislamu pamoja na wajumbe wa OIC wamealikwa kushiriki katika kongamano hilo. 650076