IQNA

Ethiopia kuanzisha benki ya kwanza ya Kiislamu

17:55 - September 08, 2010
Habari ID: 1990613
Sheria ya kuanzisha benki ya kwanza ya Kiislamu nchini Ethiopia imeidhinishwa na benki kuu ya nchi hiyo.
Kwa mujibu wa jarida la kila wiki la Capital la Ethiopia, Benki Kuu ya Ethiopia inafanya mazungumzo na benki za nchi hiyo kwa lengo la kutekeleza huduma za kibenki na kibiashara kwa mujibu wa sheria za Kiislamu.
Kwa mujibu wa sheria hiyo, benki za kitaifa na kigeni zilizo nchini Ethiopia zimeidhinishwa kutoa huduma kwa mujibu wa sheria za Kiislamu. Aidha raia wa Ethiopia wana haki ya kuanzisha Benki za Kiislamu.
650480
captcha