IQNA

Msikiti wenye umri wa miaka 1000 wazinduliwa katika haram ya Imam Ali bin Abi Twalib

15:40 - October 11, 2010
Habari ID: 2010797
Msikiti wa Umran bin Shahin ulioko kaskazini mwa haram ya Imam Ali bin Abi Twalib (sa) ambao una umri wa karibu miaka 1000 umefunguliwa tena baada ya kukarabatiwa.
Shughuli ya kufunguliwa tena msikiti huo mkongwe imehudhuriwa na Sayyid Salih al Haidari ambaye ni mkuu wa Taasisi ya Wakfu wa Shia nchini Iraq na shakhsia mbalimbali wa kidini na kielimu wa mji mtakatifu wa Najaf.
Mkuu wa kitengo cha utafiti cha haram ya Imam Ali (as) Mudhaffar Mahbuba amesema kuwa msikiti huo mkongwe una umri wa miaka 1000 na ulipuuzwa na kutelekezwa katika kipindi kirefu cha utawala ulioondolewa madarakani wa dikteta Saddam Hussein.
Amesema kuwa kitengo cha masuala ya uhandisi cha haram tukufu ya Imam Ali bin Abi Twalib (as) kimekarabati msikiti huo kwa gharama ya dinari milioni tatu za Iraq baada ya kufanya utafiti kamili na kwamba msikiti huo sasa uko tayari kupokea wasomi na watu mbalimbali kwa ajili ya ibada ya swala. 672774
captcha