Muhammad Abdallah As-Sai, mkuu wa idara ya ratiba za masomo ya kituo cha as-Sheikh Id amesema kuhusiana na suala hilo kwamba masomo hayo yamepangwa kuanza siku ya Jumapili tarehe 17 Oktoba. Amesema, masomo hayo ambayo yataendelea kwa kipindi cha miaka miwili yatakuwa yakifanyika siku za Jumapili, Jumatatu, Jumanne na Jumatano za kila wiki.
Amesema waalimu mashuhuri wamechaguliwa kuendesha shughuli hiyo ambapo masomo muhimu zaidi yatakayofundishwa ni pamoja na tafsiri ya Qur'ani, elimu ya Qur'ani, tajweedi, fiqhi na hadithi, fiqhi na nahau, usuul fiqhi, elimu ya hadithi, kanuni za fiqhi, fiqhi na sira, madhebu na kidini na madhehebu ya kiitikadi.
Khalil bin Muhammad az-Zeir, mkurugenzi mwandamizi wa taasisi hiyo amesema kwamba tayari shughuli ya uandikishaji wa majina ya washiriki wa masomo hayo imeanza na kwamba watakaohitimu watapewa cheti cha diploma ya masomo ya Kiislamu.
Wakuu wa taasisi hiyo wanasema kuwa lengo la kuanzishwa masomo hayo ni kuimarisha imani, thamani za kiutu, maadili na ufahamu wa sheria za Kiislamu katika jamii. 673867