IQNA

Mafunzo ya hija kwa Mashia wa Saudi Arabia

12:50 - October 14, 2010
Habari ID: 2012661
Ratiba ya mafunzo ya jinsi ya kutekeleza amali za hija itaanza kutekelezwa tokea siku ya Jumamosi tarehe 16 Oktoba katika Msikiti wa Rasul al-A'dham (saw) huko katika mji wa al-Mubarriz katika mkoa wa Washia waliowengi wa al-Ahsaa.
Masomo hayo ya hija tamatu' ambayo ni mahsusi kwa wakaazi wa mkoa uliotajwa yataendeshwa na wasomi pamoja na wanazuoni wa Kishia wa Saudi Arabia.
Wanafunzi wa masomo ya kidini na wataalamu wa sheria na kanuni za usomaji Qur'ani wanashiriki katika utekelezaji wa ratiba hiyo ambapo watawafundisha washiriki namna ya kusoma kwa njia sahihi Qur'ani Tukufu na dua.
Masomo hayo ambayo yatawashirikisha wanawake na wanaume yatachukua muda wa wiki nne. 674295
captcha