IQNA

Katibu Mkuu wa OIC atunukiwa nishani ya shukrani

11:48 - October 31, 2010
Habari ID: 2022258
Rais Omar Hassan al Bashir wa Sudan amemtunuku Profesa Ekmeleddin Ihsanoglu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiislamu OIC nishani ya daraja ya kwanza ya huduma zenye thamani.
Kwa mujibu wa tovuti ya OIC, Profesa Ihsanoglu alitunukiwa nishani hiyo siku ya Alhamisi baada ya kumalizika Kikao cha Tano cha Kimataifa cha Usalama wa Chakula katika nchi za Kiislamu mjini Khartoum.
Nishani hiyo imetolewa kama njia za kuyashukuru makao makuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiislamu kwa juhudi za kuuhudumia umma wa Kiislamu. Kikao hicho cha Khartoum kilidhuhuriwa na nchi 27 wanachama wa OIC pamoja na asasi 10 za kimataifa.
685260
captcha