IQNA

Mahujaji karibu milioni 2 kuhiji mwaka huu

14:14 - November 01, 2010
Habari ID: 2023506
Fuad bin Abdu Salaam al-Farisi, Waziri wa Hija wa Saudi Arabia ametangaza kwamba mwaka huu mahujaji karibu milioni mbili wanatazamiwa kutekeleza ibada tukufu ya hija, milioni 1 na laki 75 wakiwa ni wageni na laki mbili na nusu wenyeji wa Saudia.
Kwa mujibu wa gazeti la Arab News, al-Farisi amegusia suala hilo alipokuwa akizungumza katika warsha ya mafunzo ya kudhibiti umati huko Jamarat Mina na kuongeza kuwa kwa kutilia maanani idadi kubwa ya mahujaji mwaka huu, hatua muhimu zimechukuliwa kwa ajili ya kuboresha hali ya mahujaji watakapokuwa wakirusha mawe kwenye daraja la Jamarat. Amesema warsha ya mafunzo ya Jamarat itakuwa ikifanyika kila mwaka kwa lengo la kubadilishana uzoefu na habari za kuboresha hali ya mahujaji na kurahisisha harakati yao wakati wa kurushia mawe mashetani huko Mina.
Al-Farisi amesisitiza kwamba Saudia ina nia ya kutekeleza miradi zaidi katika siku zijazo kwa madhumuni ya kuboresha hali ya mahujaji katika msimu wa hija. 685830
captcha