IQNA

Mashindano ya Qur'ani ya wanawake kufanyika Tehran Novemba 17

11:56 - November 04, 2010
Habari ID: 2025345
Mashindano ya Kitaifa ya wanawake ya Kuhifadhi Qur'ani Tukufu yanatazamiwa kuanza Novemba 17 sawia na 10 Dhul Hijja, katika sikukuu ya Idul Adha mjini Tehran.
Kwa mujibu wa Muhammad Hussein Sabzali mkuu wa Kituo cha Darul Qur'an cha Imam Ali AS kinachoandaa mashindano hayo, washiriki wataweza kushindana katika viwango vitatu vya kuhifadhi Qur'ani Tukufu na vile vile Tarteel.
Amesema wanawake 160 watashiriki katika mashindano hayo ya siku tatu yatakayofanyika katika Kituo cha Kidini cha Fatimiyun mjini Tehran.
Kituo cha Darul Quran cha Imam Ali AS kimesema mashidano ya wanaume yatafanyika kwa muda wa siku tatu kuanzia Disemba 29.
686500
captcha